Biashara Yamshinda Ini Edo
Na ANDREW CARLOS| GAZETI LA IJUMAA| KUTOKA NAIJA
IMEFICHUKA kwamba mkongwe wa filamu kutoka Nollywood, Ini Edo ameshindwa biashara na kuamua kufunga klabu yake kubwa na maarufu ya Mimz iliyopo Lekki, Lagos.
Inaelezwa kuwa, klabu hiyo imedumu kwa muda wa miaka miwili tu tangu aifungue Septemba 2015 huku sababu za kuifunga ikitajwa kuwa ni uongozi mbovu kutoka kwa mtu ambaye hakutajwa jina lake.
Ini Edo ambaye licha ya kuendelea kuigiza ni mshauri wa mambo ya utalii katika Jimbo la Akwa Ibom, ameshathibitisha kusitisha biashara hiyo huku akificha chanzo chake.