The House of Favourite Newspapers

Tambwe: Yanga Inavuka Leo, Wala Msiogope

Wachezaji wa timu ya St Louis ya Shelisheli (wenye jezi nyeupe) wakipambana na wachezaji wa Yanga.

KIKOSI cha Yanga, leo Jumatano kinashuka uwanjani kupambana na St Louis ya Shelisheli katika mchezo wa marudiano wa Klabu Bingwa Afrika, huku kikiwakosa nyota wake wanne wa kigeni kutokana na majeraha

 

Kwenye mchezo huo muhimu, Yanga itamkosa, Obrey Chirwa, Amissi Tambwe, Donald Ngoma pamoja na Thaban Kamusoko.

Kikosi cha timu ya Yanga.

“Yanga hawana haja ya kuwa na wasiwasi na wache­zaji watakaocheza dhidi ya St Louis, kwani ni wacheza wa­zuri na wenye uwezo kufanya vizuri endapo wataamua kupambana.

 

“Nasema hivyo kwa sababu ninawajua vizuri, baadhi yao wana uwezo mkubwa kushinda hata sisi tuliobaki huku ila tu tunachowashinda sisi ni uzoefu lakini wakiamua kupambana ushindi utapa­tikana na ninaamini itakuwa hivyo,” alisema Tambwe ambaye amewahi kutamba na Simba.

Stori na Sweetbert Lukonge | Global Publishers

Comments are closed.