Caf Yatangaza Utaratibu Wa Kuchezesha Droo Klabu Bingwa, Shirikisho leo
Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) leo litachezesha droo ya makundi ya timu zilizofuzu kucheza Ligi ya Mabingwa makao makuu leo saa mbili usiku kwenye Hoteli ya Ritz Carlton, jijini Cairo, Misri.
Droo hizo za KlabU Bingwa zitachezeshwa kulingana na matokeo ya timu husika katika miaka mitano iliyopita kuanzia 2013 hadi 2017.
Kwa Ligi ya Mabingwa timu zimepangwa katika makundi manne ambayo ni:
Pot 1: TP Mazembe (DR Congo), Al Ahly (Egypt), Etoile du Sahel (Tunisia), Wydad (Morocco)
Pot 2: Mamelodi Sundowns (South Africa), Zesco (Zambia), Esperance (Tunisia), ES Setif (Algeria
Pot 3: MC Alger (Algeria), KCCA (Uganda), Horoya (Guinea), Mbabane Swallows (Swaziland)
Pot 4: Primero de Agosto (Angola), Township Rollers (Botswana), Difaa El Jadidi (Morocco), AS Port (Togo)
Kwa upande wa Kombe la Shirikisho makundi yamepangwa kufuatana na matokeo ya timu 32 ambazo timu hizo zimecheza katika miaka mitano iliyopita kama ifuatavyo:
Pot A: El Hilal (Sudan), Saint George (Ethiopia), AS Vita (DR Congo), Zanaco (Zambia)
Pot B: USM Alger (Algeria), Supersport (South Africa), Hilal Obied (Sudan), Enyimba (Nigeria)
Pot C: ASEC Mimosas (Cote d’Ivoire), Mounana (Gabon), Young Africans (Tanzania), Williamsville (Cote d’Ivoire), Aduana (Ghana), Gor Mahia (Kenya), UD Songo (Mozambique), MFM (Nigeria), Plateau (Nigeria), Rayon Sport (Rwanda), Generation Foot (Senegal), Bidvest (South Africa)
Pot D: CR Belouizdad (Algeria), La Mancha (Congo), CARA (Congo), El Masry (Egypt), Niefang (Equatorial Guinea), Wolaitta Dicha (Ethiopia), Fosa Junior (Madagascar), Djoliba (Mali), RS Berkane (Morocco), Raja Club Athletic (Morocco), Costa do Sol (Mozambique), Akwa (Nigeria)
Droo ya kwanza itahusisha mechi kati ya timu za Kundi A na Kundi D. Mchakato huo utarudiwa mara nne. Baadaye, timu zilizoko Kundi B zitapambanishwa na Kundi C. Mchakato huo pia utarudiwa mara nne.
Baada ya kukamilika, timu nane zilizobaki Kundi C zitapangiwa na timu zilizoko Kundi D. Timu itakayokuwa imebaki katika Kundi C itapambanishwa na timu kutoka Kundi D. Mchakato huo utarudiwa mara nane kukailisha ratiba
Comments are closed.