The House of Favourite Newspapers

Yanga wajuaji wengi, TFF wenye ‘akili’ wachache

WIKI jana nilielezea kuhu­su mazingira ya Shirikisho la Soka la Tanzania (TFF) kuhusu utendaji kazi wao, nitazun­gumzia na leo tena kidogo, lakini nimeona haitakuwa sawa wiki ikipita bila ku­toa maoni yangu kinach­oendelea ndani ya Yanga.

 

Yanga kuna wajuaji wengi Wakati Yusuf Manji akiwa kiongozi wa klabu hiyo ili­kuwa raha kwa wengi, Wa­nayanga waliamini wao ndiyo wababe wa soka la Tanzania kwa kuwa wa­likuwa na nguvu ya fedha, wakasahau fedha hizo ni za mtu binafsi na siyo klabu.

 

Mara nyingi nimewahi kusema kuwa hilo lilikuwa kosa kwa kuwa kama TFF na Shirikisho la Soka la Ki­mataifa (Fifa) wangeamua kufanya kitu kinaitwa ‘finan­cial fair play’ basi ingekuwa tatizo kwa Yanga. Manji al­iona hilo na kwa kuwa ni mfanyabiashara ndiyo maa­na alitaka abadilishe aina ya uendeshaji wa klabu.

 

Bahati mbaya halikutim­ia, kilichotokea hayupo na klabu imekuwa ikipepesuka. Wale waliokuwa wakimpin­ga na kuona anakosea nao wameingia mitini.

 

Siyo kwamba wanaoji­fanya wajuaji wa mambo ya Yanga hawajui umuhimu wa muwekezaji, wanajua lakini kwa kuwa wanataka masla­hi yao binafsi ndiyo maana kumekuwa na ugumu wa kujitokeza mtu mwingine kuwekeza klabuni hapo.

 

Inavyoonekana kuna aina ya watu ambao kazi yao wao ni kupinga maen­deleo na wanataka klabu ibaki kuendelea kulia njaa huku wao wakifaidika, wa­najua ukianza kutumika mfumo mpya wa uende­shaji basi itakula kwao.

Wakati Yanga wakiiteua ile kamati ya kina Abass Tarimba nilijua kuna kazi kubwa. Kwa akili ya kawa­ida tu jiulize, wakati kamati hiyo ikiteuliwa kufanya kazi kwa muda nini maju­kumu ya kamati ya utendaji.

 

Moja kwa moja kwa aina ya uongozi wa Kibongo wa kupenda sifa ilikuwa ngumu pande mbili kufanya kazi moja huku kila upande uki­taka kuonekana upo juu.

Kinachoiangusha Yanga hadi sasa ni kuwa kuna wajuaji wengi wa mambo, tena asilimia kubwa hu­wezi kuwaona kwenye ‘me­dia’, wao wanajiita watu wa ndani, kwa mwendo ulivyo kunahitajika mtu au watu wenye maamuzi magumu kubadili upepo, la sivyo hali inaweza kuen­delea kuwa mbaya zaidi.

 

TFF wenye ‘ak­ili’ ni wachache Wiki jana nilieleza jin­si upepo ulivyoanza kwenda kombo ndani ya taasisi hiyo inayoon­gozwa na Wallace Karia.

Niligusia mambo kadhaa ikiwemo ucheleweshwaji wa kutolewa kwa ratiba ya msimu, uhusiano wao na waandishi wa habari katika baadhi ya mambo, kuon­doka kwa Kim Poulsen, ku­kosekana kwa kocha wa Tai­fa Stars na mengine kadhaa.

 

Baada ya kusema hayo, hoja ya majaaliwa ya soka la vijana baada ya kuondoka kwa Poulsen sijajua itaku­waje, siyo kwamba hakuna kocha mwingine anayewe­za kubeba mamlaka hayo, lakini kwa kuwa Tanzania tutakuwa mwenyeji wa mi­chuano ijayo ya Afcon U-17 mwakani, ni vema tukawa na mwelekeo mzuri wa nini tu­natakiwa kufanya mapema.

Mara likaibuka suala la TFF kumuondoa Clement Sanga katika nafasi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi kwa kile kilichoelezwa kupata barua kutoka Yanga, ukijiuliza siku zote walikuwa wapi na kwa nini maamuzi hayo yaje wakati huu! Inatafakarisha.

 

Karia anaweza kuibuka na hoja kuwa wao TFF wame­pokea barua kutoka Yanga kuhusu kumtambua Manji kuwa bado ni mwenyekiti wao, inamaana siku zote hawakujua kama Sanga anakaimu? Nani alishughu­likia barua ya Manji kujiu­zulu pale TFF na walitoa majibu gani kwa Yanga?

 

Tunaelekea kuanza msimu mpya, timu za ligi kuu zipo 20, hadi leo md­hamini bado hajajulikana wanasema wapo katika mazungumzo na Vodacom, nini mipango ya klabu na TFF kwa jumla hadi sasa ambapo wanatarajia ku­tangaza ratiba huku md­hamini akiwa hajulikani.

Wakati timu zikiwa 16 ku­likuwa na malalamiko kad­haa ya chinichini kuhusu mambo kadhaa ya kifedha kwa klabu, leo hii timu zipo 20, mdhamini hajaju­likana, hizo bajeti za klabu zitapangwaje, ratiba zao zitakuwaje kama hawajui kiasi cha fedha wataka­chokuwa nacho mkononi!

Kwa mwenendo huu una­vyoenda ni kama vile wale wenye ‘akili’ yaani wanaojua nini kifanyike ni wachache kuliko wengine wengi wali­opo nje ya ngazi za juu au waliopo nje ya taasisi hiyo.

Comments are closed.