CCM Watuma Rambirambi Kifo Cha Mzee Ndejembi
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimepokea kwa mshtuko na huzuni kubwa taarifa za kifo cha Mzee Pancras Mtemi Ndejembi ambaye amekuwa sehemu ya mzee maarufu na wanaoheshimika katika Chama kada wa Chama na Kiongozi Mstaafu wa Chama na Serikali.
Ndejembi amefariki katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Dodoma alikopelekwa jana Ijumaa baada ya hali yake kubadilika ghafla.
Mtoto wa Marehemu, Edna Ndejembi amesema baba yake alikuwa anasumbuliwa na kifua kubana ambapo alilazwa katika Hospitali ya DCMC ya jijini Dodoma na kuruhusiwa juzi Alhamisi akiwa ameimarika kiafya.
Comments are closed.