Nisha, Baraka De Prince Mahaba Niue
Msanii anayefanya vizuri kwenye filamu Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’
Imelda Mtema
MWANADADA anayefanya vizuri kwenye filamu Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ na mwanamuziki wa Bongo Fleva, Baraka De Prince, wameonesha mahaba niue hadharani na kuwaacha watu midomo wazi.
Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Baraka De Prince
Nisha alianza kutundika picha ya msanii huyo kwenye ukurasa wake wa Instagram na kuonesha kuwa ndiye mpenzi wake ambapo Baraka naye alijibu mapigo kwa kuandika; “Safari ndiyo kwanza imeanza na kuna milima na mabonde ila kwa kuwa we ni kiboko, najua steling hauawi.”
Gazeti hili lilimtafuta Nisha ili kueleza ukweli juu ya hilo ambapo aliangua kicheko na kusema:
“Jamani jamani mimi ngoja ninyamaze maana najua kila kitu kimejieleza kwenye ukurasa wangu wa Instagram.”
JIUNGE NA GLOBAL BRAKING NEWS UPATE HABARI KEMKEM ZA UCHAGUZI MKUU