The House of Favourite Newspapers

Airtel yazindua Airtel 4G kuboresha mawasiliano nchini

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughuliki Uwekezaji Mheshimiwa Angellah Kairuki na  Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Bw, George Mathen wakiwa wameshika nembo  ya  Airtel 4G baada ya uzinduzi wa Airtel 4G Dodoma. kulia ni Mwakilishiwa wa katibu mkuu wizara ya ujenzi uchukuzi na mawasiano Munamu Mulemwa, kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya Airtel Bw Lekini Moleli .
Angellah Kairuki akizindua mtandao wa Airtel 4G mkoani Dodoma, Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Bw, George Mathen.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughuliki Uwekezaji Mheshimiwa Angellah Kairuki akizindua mtandao wa Airtel 4G mkoani Dodoma, Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania Bw, George Mathen na wengine katika picha wapili kutoka kulia ni mjumbe wa bodi ya Airtel Lekini Molel, Mwakilishiwa wa katibu mkuu wizara ya ujenzi uchukuzi na mawasiano Munamu Mulemwa, Mbunge wa viti maalum Mariam Ditopile.
Hafla ya uzinduzi ikiendelea.

 

 

 

 

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania leo imetangaza kuzindua huduma ya Airtel 4G ikiwa ni muendelezo wa kupanua wigo wa mtandao wake    nchini ili kutimiza dhamira yake ya kutoa huduma bora za kimtandao kwa wateja wake.

 


Akizindua huduma hiyo ya Airtel 4G leo jijini Dodoma, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anaeshughuliki Uwekezaji Mheshimiwa Angellah Kairuki alisema kuwa ni furaha kuona Airtel inatekeleza mipango ya uwekezaji na kuja na  huduma za mtandao wa Airtel 4G  kwa lengo la kukidhi mahitaji ya watanzania wote, hii ni ishara tosha inayoonesha mikakati ya kuijenga Airtel mpya itakayoendelea kutoa gawio kwa wanahisaikiwemo Serikali yetu.

 

“Nimefarijika kusikia taarifa kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Airtel kwamba Airtel inatekeleza mikakati yao ya uwekezaji wa kuboresha huduma kwa kuanzisha huduma hii ya 4G/LTE ikiwa na wigo mkubwa wa kutoa huduma za mawasiliano, mimi kama Waziri mwenye dhamana ya uwekezaji inanipa ishara nzuri ya matokeo ya mazingira mazuri tuliyoyaweka ili wawekezaji wetu nchini waweze kutekeleza majukumu yao na kulifaidisha taifa, haya yote yanafanikiwa  chini ya uongozi wa Serikali yetu ya awamu ya tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dokta John Joseph Pombe  Magufuli.

 

 

“Wote tunatambua, Airtel Tanzania na Serikali yetu waliingia makubaliano mazuri hivi karibuni kwamba serikali yetu iwe na umiliki wa asilimia 49 wa hisa ndani ya Airtel Tanzania, kutokana na makubaliano hayo pia hadi leo Airtel Tanzania imeshailipa serikali jumla ya bilioni 8 kama sehemu ya makubaliano hayo na leo hii Airtel wanatekeleza upanuzi wa mtandao, hii ndio mikakati ya kuijenga Airtel mpya ili kuendelea kuleta tija kwa shughuli za kijamii na uchumi, alisema kairuki.

 

Mheshimiwa Waziri Kairuki pia alitoa pongezi kwa Airtel kutokana na taarifa yao inayoonesha  kasi ya kusambaza huduma hiyo ya Airtel 4G  katika miji mikubwa takribani 25 ambapo leo wamewasha mtandao wa Airtel 4G mkoani Dodoma. “ Naamini ya kwamba kwa uzinduzi huu wa mtandao wa Airtel 4G, Airtel itazidi kuwa imara sana na sisi serikali tuko tayari kuwaunga mkono kwa hili”. Kairuki aliongeza.

 

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji Airtel Tanzania Bw, George Mathen alisema kuwa uzinduzi huu wa huduma ya Airtel 4G ni moja ya malengo ya muda mrefu ya kuifanya kampuni ya Airtel kuwa na uwezo wa kutoa huduma bora ukizingatia sasa ni ulimwengu wa kidigitali.

 

“ili mteja aweze kutumia huduma ya Airtel 4G anatakiwa kuwa na Simu ya Smatifoni yenye uwezo wakupokea mawimbi ya 4G na awe amewezesha laini yake ya simu kuwa ya Airtel 4G. Kupata uhakika kwamba simu yake inauwezo wa kutumia 4G piga *149*95#”

 

Mathen alisema Uwekezaji na upanuzi wa mtandao kwa kuzindua huduma za Airtel 4G ni kutelekeza makubaliano baina wa wabia wetu ambao ni serikali ya kuhakikisha ya kwamba Airtel inaendeleza uwekezaji kwenye upanuzi wa mtandao kwa lengo la kuzidi kuwa na mtandao imara.

 

Aliongeza kuwa huduma ya 4G itatoa nafasi kukuza teknolojia ya kidigitali hapa nchini kwa kuwa na huduma nafuu na zenye kasi za intaneti na hivyo kubadilisha maisha ya Watanzania. “Airtel tutaendelea kuzindua huduma na bidhaa nafuu kwa ajili ya Watanzania wa kila rika” Mathen aliongeza.

Comments are closed.