The House of Favourite Newspapers

Ajali ya basi yaua 12 na kujeruhi 22 Iringa

0

New Force (1)

Taswira kutoka eneo la ajali.

WATU 12 wamepoteza maisha huku wengine 28 wakijeruhiwa leo baada ya basi la New Force One kupata ajali eneo la Mahenge Wilaya ya Kilolo mkoani Iringa barabara kuu ya Iringa- Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Peter Kakamba amethibitisha watu 12 kupoteza maisha katika ajali hiyo. Wanane ni wanaume na wanne ni wanawake.

New Force (2)

Ajali hiyo imetokea majira ya saa nane alasiri ambapo basi la kampuni ya New Force One aina ya Youtong lenye namba za usajili T483 CTF likitoka Tunduma kwenda Dar limegongana na lori aina ya Scania lenye namba T 616 DEF katika kijiji cha Mahenge, Wilaya ya Kilolo Mkoa wa Iringa katika barabara kuu ya Iringa – Dar.

Majeruhi wa ajali hiyo wamelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Ilula, kilomita 45 kutoka Iringa Mjini.

 

Leave A Reply