KIUNGO mshambuliaji anayeongoza kwa asisti nyingi Yanga, Ibrahim Ajibu, ameibuka na kuwaambia maneno mazuri ya kuwatia matumaini mashabiki wa timu hiyo, kwa kutamka kuwa mashabiki wasihofu, mambo mazuri yanakuja.
Kauli hiyo aliitoa ikiwa ni saa chache kabla ya pambano lao dhidi ya Mbao FC katika mchezo wa Ligi Kuu Bara jana Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Ajibu alisema wao kama wachezaji wanatambua umuhimu wa mashabiki wao, hivyo ni lazima wapate matokeo mazuri katika michezo ijayo ya ligi ili kuhakikisha wanafanikisha malengo yao.
Ajibu alisema, wanafahamu ugumu wa ligi uliopo katika msimu huu, lakini watahakikisha wanafanya kila liwezekanalo kufanikisha ushindi huku akiwataka mashabiki kutokata tamaa kujitokeza uwanjani, pale wanapopata matokeo mabaya.
“Tunataka kuona timu yetu ikiendelea kupata matokeo mazuri,” alisema Ajibu.
Wilbert Molandi, Dar es Salaam.
Comments are closed.