The House of Favourite Newspapers

Aliyepiga Picha za Mauaji ya Mwangosi Afariki

0

Senga

Mpiga picha wa Gazeti la Tanzania Daima, aliyepiga picha za tukio la mauaji ya Mwangosi Joseph Senga enzi za uhai wake.

Na Dotto Bulendu

NI simanzi na majonzi, siku moja baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Iringa kumhukumu kifungo cha miaka 15 askari aliyemuua mwandishi Daudi Mwangosi, tasnia ya habari imepata pigo kwa kuondokewa na mpiga picha wa Gazeti la Tanzania Daima, aliyepiga picha za tukio la mauaji ya Mwangosi, SHUJAA JOSEPH SENGA, aliyefariki dunia jana usiku.

Senga amefia nchini India alikopelekwa kwa matibabu ya ugonjwa wa moyo.

mwangosi 2

Mojawapo ya picha za tukio la mauaji ya Mwangosi alizopiga Joseph Senga.

Bila Joseph Senga, shujaa aliyehatarisha maisha yake, akasimama bila woga, akapiga picha akiwa katikati ya msitu wa askari polisi wenye silaha, huku anga ikiwa imegubikwa na moshi wa mabomu ya machozi, milio ya risasi ikisikika na kuzitunza, zikasaidia kufichua mauaji ya Mwangosi, leo hii asingekuwa Senga, nadhani kusingekuwa na kesi na mwisho hukumu dhidi ya aliyemuua Mwangosi. Nakulilia Senga.

mwangosi

Daudi Mwangosi enzi za uhai wake.

Senga, Senga, Senga, Senga, umekwenda, Mungu aliamua akuweke hai mpaka hukumu itoke na mwisho amekuchukua, Senga umekwenda wadogo zako katika tasnia tukiwa na hamu ya kujifunza kutoka kwako.

Senga, Senga, kamsalimie Daudi Mwangosi, mwabie aliyemuua naye kahukumiwa jela miaka 15, kamwambie mazingira ya waandishi wa habari bado magumu.

Nenda Senga, picha zako zinabaki kuwa rejea ya mafunzo ya uandishi wa habari katika mazingira hatarishi.

Leave A Reply