The House of Favourite Newspapers

Amunike kaa mguu sawa, sisi Watanzania ni Wabrazili

MWAKA 2001, timu ya taifa ya Brazil ilikuwa kwenye hatikati ya kuko­sa michuano ya Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza kutokana na mwenendo wa kusuasua wa timu hiyo.

Inajulikana wazi kati ya nchi yenye presha kubwa ka­tika mchezo wa soka kuliko zote ni Brazil, kuna sababu kubwa kama tatu hivi, kwan­za ni vipaji vingi walivyona­vyo, pili ni wingi wa watu wa taifa hilo (inakaridiwa wapo zaidi ya watu milioni 200) na tatu ni kuwa kila mtu ni kocha kwenye taifa hilo.

Kuna wakati ilifika hatua un­aweza kupanga vikosi vitano vya taifa la Brazil na vyote vikawa bora na vinaweza ku­fika fainali ya Kombe la Dunia.

 

Juni 2001, Luiz Felipe Scolari aliteuliwa kuwa ko­cha wa taifa hilo, presha ili­kuwa kubwa, alianza mch­ezo wa kwanza vibaya kwa kufungwa na Uruguay bao 1-0, baada ya hapo akaen­delea vizuri na mwisho aka­tangaza kumuacha kikosini ‘Mungu’ wa soka wa wakati huo kwa Wabrazili, Romário.

Ilikuwa ngumu kwa Wa­brazili kumuelewa kwa kuwa waliamini Romario ndiye kila kitu kwao. Baadhi ya mashabiki wakamwambia anapoenda kushiriki ka­tika Kombe la Dunia, ahak­ikishe anarejea na taji, kinyume na hapo apande ndege apitilize anapopa­jua na siyo kurejea Brazil.

 

Scolari aliuvaa moyo wa paka, akaenda na kube­ba kombe akarejea kifua mbele, chuki yote ikapotea na akaonekana ni shujaa.

Stori hiyo nimeisimulia ili iendane na kile ambacho ni­takizungumza hapa, Kocha wa Taifa Stars, Mnigeria, Emmanuel Amunike ame­kuwa na misimamo kama ya Scolari kwa kiasi fulani licha ya kuwa ana muda mfupi tangu awe bosi wa timu hiyo.

 

Katika mchezo dhidi ya Uganda kuwania kufuzu Af­con 2019, aliwaacha wache­zaji wa Simba kwa kile kili­choelezwa kuwa walichelewa kuripoti kambini, japokuwa baadaye ilibainika kulikuwa na tatizo la mawasiliano na ndiyo maana kiongozi mmoja akachukuliwa hatua, Amunike hakutaka kubadili maamuzi, akashikilia msimamo wake.

Taifa Stars ikaam­bulia matokeo ya 0-0 ikiwa na wachezaji wen­gi ambao awali hawaku­wemo katika mipango.

 

Stars ilipoenda kucheza na Cape Verde, Amunike pia akafanya maamuzi ya kumuacha pembeni beki mkongwe Kelvin Yondani kwa sababu anazozijua yeye, pengo likaonekana na timu ikapoteza kwa mabao 3-0.

Aliporejea nchini akareke­bisha makosa na timu ika­pata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya haohao Cape Verde. Mchezo wa juzi dhidi ya Lesotho, Stars ilionekana kuwa na kikosi ambacho wengi walikishangaa na ndiyo maana hata baada ya kupoteza lawama zime­kuwa nyingi kwa kocha huyo.

 

Sikuwepo kambini lakini pia kilichotokea baadaye ni kuwa kulikuwa na maneno mengi kuhusu mvurugano kambini.

Nikukmbushe kitu kimoja, wiki chache wakati akiwa hotelini anapoishi, Amunike aliwahi kuulizwa na gazeti hili sababu za kutomuita kiko­sini Ibrahim Ajibu wa Yanga ambaye kwa miezi ya hivi karibuni amekuwa akionye­sha kiwango cha juu na kwa kuwa soka halichezwi chum­bani kila mtu ameliona hilo.

 

Sehemu ya majibu yake alisema hivi: “Nani Ajibu? Ndiyo nani huyo? Kwani mchezaji yuko peke yake? Wapo wengine wanaofaa zaidi yake na kuna wache­zaji wengi tu ninaoweza kuwaita siyo lazima yeye.”

Kauli hiyo ilinishangaza kidogo na sikutegemea ku­tolewa na mtu mwenye uzoe­fu mkubwa katika soka kama Amunike ambaye kama ni ile hali ya kuwa ‘profesheno’ ili­kuwa sehemu ya maisha yake.

Hilo likapita na sasa kuna tetesi kuwa alivuru­gana na baadhi ya wache­zaji kambini na ndiyo maa­na wengine hakuwapanga.

 

Katika soka, Tanzania li­cha ya kuwa hatuna ma­faniko makubwa lakini uk­weli ni kuwa tuna tabia kama za Wabrazili, tunajua kumpa mtu presha, tuna­jua kumpamba mtu tukia­mua na tunajua kumvuruga tena sana kama tukiamua.

Rekodi za ukocha zinaonye­sha Amunike pamoja na kucheza soka kwa kiwango cha juu hajawahi kukutana na kazi kubwa na yenye presha kama hii, kwa kuwa alikuwa ni kocha wa timu za vijana au msaidizi miaka ya nyuma.

 

Kuajiriwa kuwa kocha wa Stars ni wazi ni cheo chake cha kwanza kikubwa tangu aanze majukumu ya ukocha, yawezekana akaifanya kuwa sehemu ya kujifunza kwake lakini wale mliopo karibu naye mfikishieni ujumbe kuwa sisi Watanzania ni Wabrazili, aki­taka atufunge mdomo afanye yale aliyoyafanya Scholari.

JOHN JOSEPH

WEMA Alivyotinga Mahakamani Tena, Kesi ya Video za Ngono!

Comments are closed.