The House of Favourite Newspapers

ARUSHA: Lema Akamatwa na Polisi

Picha na maktaba.

JESHI la Polisi mkoani Arusha limemkamata Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema  kwa madai ya kuzidisha muda wakati akihutubia kwenye mkutano wake na wananchi jana Jumatano, Agosti 23, 2017 jijini humo.

Polisi wamedai kuwa Lema alimaliza mkutano wake saa 12:7 jioni badala ya saa 12:00 kama ilivyo utaratibu.

Hivyo askari polisi walimzuia katika mzunguko wa barabara wa Mnara wa Saa (round about) kwa kusimamisha gari mbili (moja mbele na nyingine nyuma), kisha kuingia katika gari yake na kumuelekeza Kituo Kikuu cha Polisi (Central Police) mjini Arusha.

Taarifa zaidi, endelea kufuatilia mitandao yetu.

Comments are closed.