The House of Favourite Newspapers

Baba Levo Akerwa na Diamond, ‘Ameleta Udini’

0

MSANII wa muziki wa Bongo Fleva na diwani wa kata ya Mwanga kaskazini Baba Levo amefunguka na kuonyeshwa kukerwa na baadhi ya vitu vilivyotokea mkoani Kigoma katika show ya Diamond ya kuazimisha miaka 10 yake kwenye tasnia.

 

Baba Levo ameonyeshwa kukerwa na Diamond huku akisema; “Diamond alifanya makosa mawili makubwa na sisi huwa ni wasema kweli pale linapotokea jamboi, tatizo la kwanza ni kwa baadhi ya wasanii kutopanda jukwaani na kufanya show na hiyo ndio ilipelekea fujo nyingi mpaka watu wakaanza kurusha mawe.

 

“Tatizo la pili ni kujenga msikiti na madrasa kwani aliangalia kwa upande wa waislamu tu, hilo amefanya Udini, basi angejenga Kanisa ili kuleta usawa, mimi nilimshauri ajenge soko maana kuna akina mama kama mia nne hivi wanapata shida na hapo wanenda watu wote Wakristo, Waislamu lakini akakataa,” amesema Baba Levo.

 

Leave A Reply