The House of Favourite Newspapers

Baba P… Baba Pili… Baba Pilima!-15

1

ILIPOISHIA IJUMAA WIKIENDA:
Kabla mama Pilima hajafunguka simu ya baba Pili iliita, aliyepiga ni baba Pilima kwani aliseviwa kwa jina la Emmanuel…

“Subiri kwanza nimsikie huyu mgeni aliyeoondoka,” aliomba baba Pili…
“Haloo bwana Emmanuel…”
“Mimi si Emmanuel, naitwa Marco au baba Pilima…”
SASA ENDELEA…

Baba Pili alikata simu ghafla, akamtumbulia macho mama Pilima…
“Ina maana huyu jamaa ni mumeo?” alimuuliza mama Pilima…
“Ndiyo,” mama Pilima alijibu kwa mkato.
“Mh! Usitake kuniambia mama Pilima. Ina maana amejua kila kitu?” aliuliza tena baba Pili…

“Siyo amejua kila kitu, bali nahisi amepanga kufanya hivi…we unafahamiana naye?” mama Pilima alimuuliza baba Pili…
“Simfahamu…yaani ilikuwa hivi…”

Baba Pili alianza kumsimulia kila kitu mama Pilima huku akionekana kuwa na wasiwasi sana. Mama Pilima naye alikuwa na wasiwasi mkubwa. Kwanza alijua mume wake hakwenda mbali na angerudi kwa njia ya fumanizi sasa.

Hivyo alikuwa na mchecheto…
“Sasa mimi naona niondoke zangu,” alisema mama Pilima huku akisimama. Ni baada ya maelezo ya baba Pili ambapo ilibainika wawili hao siyo watu wanaojuana, hivyo mama Pilima akajua kuna kitu.***

Baba Pilima alipotoka hapo alimpigia simu baba Pilima feki…
“Mambo ndugu yangu?”
“Poapoa, nani mwenzangu?”
“Mimi naitwa Juma Ally. Namba yako nimepewa na rafiki yako, anaitwa Juma kama mimi…uko wapi nikuone? Nina biashara nataka kufanya na wewe!”

Alipoulizwa hivyo, awali alijiuliza Juma Ally alikuwa nani na alitaka kufanya naye biashara gani, hakupata jibu.
Kwa kuwa alipozi sekunde kadhaa bila kuendelea kuzungumza na aliyempigia simu, baba Pilima akamwambia;

“Vipi ndugu yangu mbona huzungumzi, muhimu sana tuonane leo kwani kesho natarajia kusafiri.”

Baba Pilima feki alipoambiwa hivyo akaona kabla ya kuendelea na mazungumzo amwulize ni Juma yupi aliyempatia namba yake;
“Oke…namba yangu amekupa Juma yupi? Maana kuna Juma wa Kimara na Juma wa Mbezi Beach!”

“Mh! Yule sijajua anaishi Mbezi ipi!”
“Anyway, wewe njoo mpaka Buguruni, kuna baa inaitwa Sewa, mimi nipo hapa.”
“Hapo Sewa unatarajia kukaa kwa muda gani maana nipo mbali kidogo?” baba Pilima feki alimwuliza.
“Mimi nitakusubiri muda wowote, kikubwa nataka kuonana na wewe leo,” baba Pilima alimwambia.

“Sawa.”
Baba Pilima aliharakisha kufika Buguruni mpaka kwenye baa hiyo, akazama ndani na kumkuta baba Pilima mwenzake amekaa na washkaji wake watatu, akiwemo Juma mmoja.

Baada ya salamu, baba Pilima feki akasema…
“Sasa wewe namba yangu utakuwa umepewa na Juma wa Mbezi Beach, maana Juma wa Kimara ni huyu hapa…”
“Oke…oke…oke! Sawa.”

“Sasa jamani ngoja nikae na mgeni wangu pembeni kidogo,” alisema baba Pilima huku akisimama, akaenda kukaa meza nyingine na baba Pilima mwenyewe…
“Enhee, niambie ndugu yangu…ulisema unaitwa..?”
“Juma Ally.”
“Haya Juma Ally niambie.”

***
Mama Pilima kule Kariakoo hakupenda kurudi nyumbani bila kukutana na mumewe kwanza na kuzungumza naye ili ikibidi mambo yaishe ndipo aweze kufika nyumbani…
“Yaani bila kumaliza haya mambo sidhani kama nitaweza kurudi nyumbani. Hali yangu itakuwa mbaya mimi,” alisema moyoni mama Pilima. Alimpigia simu…

“Sorry… ngoja nipokee simu ya mke wangu kwanza,” alisema baba Pilima…
“Oke…oke…”

Baba Pilima alimpokelea mkewe…
Lakini wakati huohuo, simu ya baba Pilima feki iliita, aliyepiga ni baba Pili, pacha wake. Alitaka kumpasha kilichomtokea lakini baba Pilima feki hakupokea kwa sababu baba Pilima au Juma Ally alikuwa akiongea na mkewe, akamtumia meseji…
“Nitakupigia niko na mgeni wangu mara moja.”

“Poa,” alijibu baba Pili…
“Uko wapi baba Pilima?” mama Pilima alimuuliza mke wake…
“Niko Buguruni…”
“Naomba nije tuonane please…”
“Njoo.”

“Oke, Buguruni sehemu gani?”
“Kuna baa inaitwa Sewa.”
“Poa.”
Baba Pilima mwenyewe alimshukuru Mungu wake akijua amemaliza kazi maana mkewe amejiingiza mwenyewe kwenye mtego wake…
“Enhe, niambie bwana Juma,” alisema baba Pilima feki huku akikaa sawasawa au akikaa vizuri.

“Mimi ninashughulika na biashara ya mbao, sasa niliambiwa wewe unajua wateja wanaolipa sawasawa…sijui ni kweli?” alianza kusema baba Pilima mwenyewe.
Baba Pilima feki alimtumbulia macho pima, maana yeye si mfanyabiashara kabisa, sasa hata kama ni kweli alipewa namba na Juma wa Mbezi Beach, mbona naye anajua yeye si mfanyabiashara!!

“Da! Umenipeleka mbali sana bwana Juma Ally…kwanza kama kweli Juma ndiyo amekupa namba yangu mbona anajua mimi siyo mfanyabiashara au alikosea akakupa namba yangu?”

“Mimi sijui,” alijibu baba Pilima mwenyewe. Alishaanza kuwa na wasiwasi sasa.
Akashika simu yake na kuandika namba za rafiki yake Juma wa Mbezi Beach ili amuulize kisa cha kutoa namba yake kwamba anawajua wateja wa mbao wakati anajua yeye si mfanyabiashara.

Baba Pilima mwenyewe alitaka kumzuia, lakini moyoni akasema aache tu, atapambana mpaka mwisho na vile mkewe yuko njiani, mshindi atakuwa yeye tu…
“Haloo Juma…” alianza kwa kuita baba Pilima feki…

Je, unajua nini kilitokea hapo? Usikose kusoma kwenye Gazeti la Ijumaa Wikienda, siku ya Jumatatu.

1 Comment
  1. Nesphory Ntuyahaga says

    Duh!
    Utamu kolea kweli.

Leave A Reply