The House of Favourite Newspapers

Balozi Nchimbi Apokea na Kujibu Maswali ya Wananchi Mbozi

0
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi, akisikiliza na kujibu maswali ya wananchi mbalimbali waliojitokeza barabarani kumsalimia wakati akiwa njiani, eneo la Mlowo, Mbozi, wakati akitokea Vwawa, Mbozi, kuelekea Mbalizi, mkoani Mbeya tayari kuanza ziara ya siku 2 mkoani humo, leo Jumanne, Aprili 16, 2024, baada ya kumaliza ziara yake ya siku mbili pia, mkoani Songwe. Dk. Nchimbi, ambaye ameambatana na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) Taifa, Oganaizesheni,  Issa Haji Usi Gavu na Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Gabriel Makala, yuko katika ziara ya mikoa 6 ya Katavi, Rukwa, Songwe, Mbeya, Njombe na Ruvuma.
Leave A Reply