The House of Favourite Newspapers

Basi la Simba SC Lawekwa Sokoni

0

MWAKA mpya na mambo mapya ndani ya kikosi cha Simba, mara baada ya kuliweka sokoni basi lao la timu ambalo wamekuwa wakilitumia kwa zaidi ya miaka mitano sasa.

 

Viongozi wa Simba wameyasema hayo baada ya kusambaa picha mitandaoni zikionyesha basi jipya likiwekwa stika zenye nembo za klabu hiyo.

 

Mtendaji Mkuu wa Simba, Barabara Gonzalez aliliambia Championi Jumamosi kuwa, wapo kwenye mpango wa kubadilisha basi hilo na kununua jipya, hivyo wameliweka sokoni basi lao la sasa ili wapate fedha ya kuongezea gharama za kununua basi jipya.

 

“Unajua hata ukitaka kununua simu mpya, lazima uuze ile ya zamani kwanza, kisha uongeze hela za kununua hiyo simu. Ndiyo tulichokifanya sisi tunataka kuliuza basi letu la zamani ili tununue jipya,” alisema Barbara

STORI: ISSA LIPONDA NA MARCO MZUMBE

Leave A Reply