The House of Favourite Newspapers

Basi Lamgonga Wastara, Mama Yake Aambiwa Amefariki

0
Staa wa Bongo Muvi, Wastara Juma.

 

ILIPOISHIA…

MPENZI msomaji kama ndiyo umeanza kufua­tilia simulizi hii ya mai­sha ya staa wa Bongo Muvi, Wastara Juma bado hujachelewa.

Ni wiki ya pili tu Wastara anasimulia juu ya simulizi ya kusi­simua ya maisha yake na wiki iliyopita ali­simulia namna masaibu kwenye maisha yake yalivyoanza kumpata tangu akiwa tumboni mwa mama yake.

Alisimulia wakati mama yake akiwa na ujauzito wake wa miezi sita tu wachawi walim­tokea na kumtaka yeye aliyekuwemo tumboni.

Wastara akasimulia pia kuwa hakunyonya maziwa ya mama yake kama watoto wengine kutokana na mama yake kuugua sana baada tu ya kujifunga, akasimulia pia nam­na alivyougua sana Ugonjwa wa Kifadulo na kuishia kusimulia alivyopata ajali mbaya ya pikipiki ambayo ili­mfanya kuwa mlemavu na kwa muda wa miaka miwili akawa anasota chini!

…SASA ENDELEA

“MAMA na ndugu zangu walifahamu kuwa ndiyo hivyo tena ningemaliza maisha yangu nikiwa na­sota chini, ndiyo maana nilisimulia wiki iliyopita kuwa walinirudisha ny­umbani na nikaendelea kupata tiba za kienyeji.

“Hata hivyo, zilinisaidia kwa kiasi kikubwa maana baada ya miaka miwili ni­kiwa nasota chini nilianza kusimama kama mtoto mdogo anayejifunza kutembea. Nilikuwa niki­simama na kudondoka na baadaye nikaanza kutem­bea kwa kushika ukuta la­kini nikiuachia nadondoka chini.

Wastara Juma akiugulia.

 

“Hali hiyo nayo iliende­lea kwa muda wa mwaka mmoja ndipo Mungu al­iponisaidia nikaweza ku­fanikiwa kurudi kwenye hali yangu ya kawaida ya kutembea kabisa na hati­maye nikaanza kukimbia,” anasimulia Wastara.

Anaendelea kusimulia kuwa baada ya kupona mama yake alimsafiri­sha pamoja na kaka yake mpaka Mlandizi ambapo kulikuwa ni maskani ya bibi yake mzaa mama. Wastara anasimulia kuwa walielekea huko kwa ajili ya kushiriki Mfungo wa Mwezi wa Ramadhani.

“Sasa katika siku ya kwanza ya mfungo as­ubuhi bibi alituambia na kaka yangu tusifunge na tuanze siku iliyofuata. Tu­likubali na jioni yake alitu­tuma kufuata mabarafu ya kugandishia juisi kwenye mji wetu mwingine ambao ulikuwa juu kidogo ya pale bibi alipokuwa anaishi.

“Mbali na kututuma na­kumbuka bibi alitupa fed­ha, ambayo kama sikosei ilikuwa ni kama shilingi kumi hivi ambapo mimi na kaka yangu tuliga­wana shilingi tano – tano . Tukiwa njiani nilimwam­bia kaka yangu fedha zetu zote tuz inunul ­ie mapo­chopo cho na tule.

“Akaniuliza kwa nini nikamwam­bia nilitaka tuzimal­ize kabisa maana njiani tungegongwa na gari na tus­ingeweza kupa­ta muda wa kuzitumia tena. Kaka yangu alikataa akani­ambia kama mimi ninanunua basi ninunue lakini yeye angenunua baadaye na tusingeweza kugongwa na gari,” anasimulia Wastara na kuendelea kuwa;

“Nilimsisitiza juu ya hilo lakini aliendelea ku­kataa, nikaamua kununua kwa upande wangu. Na­kumbuka nilinunua mae­mbe, machungwa, miwa na vitu vingine kibao nikajaza kwenye gauni langu la bwanga ambalo nilikuwa nimevaa. Kaka naye aliniomba tu­kawa tunatembea huku tunakula.

“Sasa ile tunaendelea kutembea kuna sehemu tulifika tukatakiwa kuvuka barabara. Tukiwa hapo kabla ya kuvuka kuna mwanaume naye alifika na alikuwa anaendesha baiskeli. Alipotaka kuvuka alisimama kuangalia huku na huko na sisi tukashika baiskeli ili kuvuka naye.

“Akaendelea kuongoza huku tumeshika kitako cha nyuma lakini alipofi­ka katikati ya barabara alituacha na kuanga­lia pembeni yetu kuna kosta (basi dogo aina ya Toyota Coaster) li­likuwa linakuja kuto­kea Dar likafika na kutupitia PUUU, kaka yangu akarushwa up­ande mwingine na mimi nikarushwa mbele barabarani kwenye lami.

“Lile kosta likawa bado lina endelea kuondoka, likanikuta mbele na kuanza ku­niburuza chini kiasi kwamba sehemu ya kichwani nikapasuka na likanichuna kabisa sehe­mu kubwa ya ngozi ya uso.

“Sasa kwa upande wa kaka yangu kule alikodon­dokea alivunjika miguu yote miwili, lakini hakuwe­za kugundua mara moja kwa hiyo hata alipodon­doka aliinuka na kuanza kulikimbiza kosta huku akilia kutaka aonyeshwe mdogo wake alikuwa wapi lakini kabla hajafika po­pote alidondoka chini.

“Hata hivyo, kwa ba­hati nzuri pale karibu na tulipopatia ajali kulikuwa na duka la dada yetu kwa hiyo aliona namna tu­livyogongwa akaja ana­kimbia huku analia, watu wakajaa na pia dereva wa kosta hawakukimbia zaidi walielekea kuripoti kwenye Kituo cha Polisi kuwa wamegonga watoto na mmoja ambaye ni mimi alikuwa amefariki.

“Mama naye alipewa taarifa hizohizo, mama yangu alilia mno kusikia nimefariki, ndugu pia wal­iumia sana kwa taarifa hiyo, ikabidi waje hospi­tali ambako tulisaidiwa na wasamaria wema kujua hali ya yule waliyeambiwa yupo hai!”

Je, nini kitaendelea? Usikose wiki ijayo.

 

INSTALL GLOBAL PUBLISHERS APP sasa usipitwe na matukio
PAKUA HAPA==>GLOBAL PUBLISHERS APP

FULL VIDEO; Mapambano Ngumi za Global TV – Ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Tanzania Bingwa

Leave A Reply