The House of Favourite Newspapers

Benki ya CRDB Yaingia mkataba na TFF kudhamini Kombe la Shirikisho

0
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela (CRDB Bank Federation Cup) wakisaini mkataba wa udhamini wa Kombe la Shirikisho (CRDB Bank Federation Cup) wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 3 kwa miaka mitatu na nusu.

Benki ya CRDB imeingia mkataba rasmi na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ambapo itatoa zaidi ya shilingi Billioni tatu kudhamini
Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania maarufu
Kombe la FA.

Rais wa TFF Wallace Karia amewaambia waandishi wa habari mkoani Dar es Salaam kuwa mkataba huo utakuwa ni wa miaka mitatu.

Amesema kutokana na CRDB kudhamini Kombe la FA sasa litaitwa
CRDB Bank Federation Cup.

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela wakibadilishana mkataba wa udhamini wa Kombe la Shirikisho (CRDB Bank Federation Cup) uliosainiwa leo Makao Makuu ya CRDB, Dar es Salaam, mkataba huo una thamani ya zaidi shilingi bilioni 3 kwa miaka mitatu na nusu.
Matukio mbalimbali wakati TFF na CRDB wakisaini mkataba wa udhamini kwenye Kombe la Shirikisho (CRDB Bank Federation Cup) wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 3 kwa miaka mitatu na nusu.
Matukio mbalimbali wakati TFF na CRDB wakisaini mkataba wa udhamini kwenye Kombe la Shirikisho (CRDB Bank Federation Cup) wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 3 kwa miaka mitatu na nusu.
Leave A Reply