The House of Favourite Newspapers

Bi. Samia Suluhu amnadi Dk Magufuli, Serengeti na Mwibara

0

Baadhi ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza kumsikiliza Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) katika mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika katika Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda, jana.

Sehemu ya wananchi wakiwa katika mkutano wa mgombea mwenza wa CCM, Jimbo la Mwibara.

Mgombea ubunge wa Jimbo la Mwibara, Alphaxard Kangi Lugola akiwahutubia wanaCCM na wananchi wapenzi wa chama hicho waliokuwa katika mkutano wa kampeni wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Suluhu jana Jimbo la Mwibara.

Mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu Hassan akizungumza na wananchi na wanaCCM Mji wa Mugumu, Wilaya ya Serengeti jana. Ambapo katika hotuba yake amewahakikishia wananchi wa eneo hilo kuwa muda mfupi baada ya kuingia madarakani atatoa maelekezo kwa waziri wa kazi kuhakikisha makampuni yaliyowekeza Serengeti yanatoa ajira bila upendeleo huku wakizingatia kutoa kipaumbele kwa wanaSerengeti.

Wananchi na wanaCCM Mji wa Mugumu, Wilaya ya Serengeti wakiwa kwenye mkutano wa kampeni.

Mmoja wa mwangalizi maalumu wa masuala ya Uchaguzi Mkuu akiendelea na kazi katika mkutano wa kampeni wa CCM uliofanyika Mugumu jana.

Baadhi ya wananchi wa Jimbo la Mwibara wakiwa wamemsimamisha njiani mgombea mwenza wa CCM, kusikiliza kilio chao njiani alipokuwa akielekea katika mkutano wa kampeni. Wananchi hao kilio chao ilikuwa ni kuiomba Serikali iharakishe mchakato wa kuipa hadhi ya wilaya Jimbo la Mwibara ili kusogezewa huduma anuai.

Mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) akiwahutubia baadhi ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza katika mkutano wa hadhara wa kampeni uliofanyika katika Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda.

Sehemu ya umati katika mkutano wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) akiwahutubia baadhi ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza katika mkutano wa hadhara Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda.

Sehemu ya umati katika mkutano wa mgombea mwenza wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) nafasi ya urais, Bi. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) akiwahutubia baadhi ya wanaCCM na wananchi waliojitokeza katika mkutano wa hadhara Jimbo la Mwibara, Wilaya ya Bunda.

Sehemu ya msafara wa mgombea mwenza wa CCM, Bi. Samia Suluhu pamoja na viongozi, wa CCM wakiwa meza kuu.

Imeandaliwa na mtandao wa thehabari

Leave A Reply