Kheli Samil aka Mr Blue
Stori: Boniphace Ngumije
Rapa anayefanya poa Afrika Mashariki, Jackson Ngechu Makini ‘Prezzo’ kutoka nchini Kenya juzi kati alitua Bongo kwa shughuli zake za kimuziki ambapo alipata nafasi ya kukutana na mkali wa michano kutoka JPM Land, Kheli Samil aka Mr Blue na kuingia naye Studio ya THT kuandaa ujio mpya hali ambayo itambust mwanamuziki huyo ambaye ameonekana kupotea kimuziki.
Msanii Jackson Ngechu Makini ‘Prezzo’.
Blue kwa sasa anafanya poa na ngoma yake iitwayo Baki na Mimi tofauti na Prezzo ambaye ni kitambo kidogo kuwika Kibongobongo hivyo ujio wao kwa sasa utawashitua wengi na kumuinua upya Prezzo.
Prezzo amewahi kufanya vizuri alipokuwa akishirikiana na msanii AY na kufanikiwa kuteka hisia za Wabongo wengi ambapo kwa sasa amepotea.