Chama cha Wanawake Watasnia ya Filamu Tanzania (CWTF) , leo wameongoza zoezi la uchangiaji wa damu katika Stendi ya Mabasi ya Ubungo jijini Dar.
Akizungumza na GPL Mwenyekiti wa CWTF, Vanita Omary alisema kuwa, lengo la chama chao ni kufanya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo kuchangia damu.
“Leo WCTF tumezindua rasmi kampeni ya kuchangia damu na zoezi hili litafanyika kwa wiki nzima hadi Januari 11 kwa kuzunguka maeneo mbalimbali ya viunga vya Jiji la Dar, huku kilele cha zoezi hilo itakuwa ni Januari 13, 2018 katika Viwanja vya Biafra Kinondoni jijini hapa.
“Katika kuhitimisha zoezi hilo, kutakuwa na huduma mbalimbali ikiwemo Upimaji wa Kansa ya Shingo ya Kizazi, matiti, Ushauri wa uzazi salama na upimaji wa virusi vya ukimwi na ushauri nasaha. ambavyo vitatolewa bure,” alisema Vanita.
Baadhi ya wasanii waliofika katika zoezi hilo ni Nikita, Recho Mwigoha, Badra, Sabrina, Adefina, Nandy wa Jumba, lucknessy, Ruby, Vivian, Dina, Miriama, Melania na wengineo, huku Msanii wa Filamu, Kupa akiwa ndiyo MC wa Shughuli hiyo. Zoezi hilo limeandaliwa na WCTF kwa kushirikiana na Damu Salama, Umati na Jhpiego.
Na Mwandishi Wetu/GPL
Comments are closed.