MWILI wa aliyekuwa mpigapicha wa magazeti ya serikali (TSN), Athumani Hamisi Msengi, unatarajiwa kuzikwa leo Januari 5 mchana katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam baaya dua iliyofanyika katika Msikiti Uliopo Sinza Madukani, Mtaa wa Namnani.
Msengi alifariki jana asubuhi katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa akipatiwa matibabu.
Msiba huo upo nyumbani kwa marehemu Sinza-Madukani, Mtaa wa Weruweru, Nyumba namba 26 ambapo mamia ya waombolezaji wakiwemo viongozi wa Serikali walioongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul makonda, wanahabri, ndugu jamaa na marafiki wamejitokeza kwa ajili ya kumsindikiza Msengi katika safari yake ya mwisho.
NA RICHARD BUKOS | GPL
Comments are closed.