Mawaziri sita waapishwa Ikulu, Dar!
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Dkt. John Pombe Magufuli leo amewaapisha mawaziri na naibu waziri, Ikulu jijini Dar es Salaam. Rais Magufuli aliwateua mawaziri na naibu waziri hao Desemba 23 ili kukamilisha idadi kwenye Baraza la Mawaziri.
Walioapishwa leo ni
Prof. Jumanne Maghembe -Waziri wa Maliasili na Utalii.
Dkt. Philip Mpango – Waziri wa Fedha na Mipango (Ni baada ya kumteua kuwa Mbunge).
Eng. Gerson Lwenge – Waziri wa Maji na Umwagiliaji.
Dkt. Joyce Ndalichako – Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi. (Ni baada ya kumteua kuwa Mbunge)
Mh. Hamad Masauni –Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Prof. Makame Mbarawa –Aliyehamishwa kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji na kwenda Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.