The House of Favourite Newspapers

Chamberlain Kapeleka Mikosi Liverpool

0

DIRISHA la usajili wa Ulaya lilifungwa tangu Agosti 31, mwaka huu, kabla ya kufungwa usajili ul­iowashangaza wengi ni Liver­pool kumsajili kiungo msham­buliaji Oxlade-Chamberlain kutoka Arsenal.

 

Alisajiliwa kwa ada ya pauni mil­ioni 35, lilionekana ni dau kubwa huku sababu hasa ya kuhama kwa mchezaji huyo ni kama haikuwaingia watu wengi ak­ilini.

Moja ya sababu iliyosaba­bisha mchezaji huyo kuon­doka Arsenal ni kitendo cha kocha wa timu hiyo, Arsene Wenger kum­tumia katika nafasi ya kushambulia akitokea pembeni wakati yeye anataka kucheza ka­tikati.

 

Kingine ambacho kilionekana kuwa ki­mechangia uhamisho wake ni kitendo cha Arsenal kukosa na­fasi ya kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya (Uefa) huku Liverpool ikipata nafasi hiyo.

 

Kabla ya uhamisho wake huo, Arsenal ilikutana na kichapo cha mabao 4-0 kutoka kwa Liverpool katika Premier League, kipi­go hicho inawezeka­na kilinogesha maa­muzi ya Chamberlain kuamini kuwa Liver­pool ni sehemu sa­hihi kwake.

 

Kabla ya Arse­nal kupata kipigo kutoka kwa Liver­pool pia ilikuwa imetoka kupokea dozi kutoka kwa Stoke City, hivyo ikaonekana kama Arsenal inapoteza dira mapema tu mwa msimu huu wa 2017/18.

 

Baada ya Chamberlain ku­chukua maamuzi ya kuhama Arse­nal, inavyooneka­na ni kama kibao kimegeuka, kwani tangu atue Liv­erpool hali ya mambo bado im­ekuwa mbaya kwa mchezaji huyo na kwa timu yake kwa jumla.

 

Tangu Chamberlain atue Liverpool timu hiyo haijapata ushindi wowote wakati ambapo Arsenal wao hawajapoteza mchezo wowote tangu kuondoka kwake.

 

Kipigo ambacho Liverpool im­ekipata cha mabao 2-0 kutoka kwa Leicester na kuiondoa timu hiyo katika michuano ya Carabao Cup, Jumanne iliyopita kimeendelea kumpa presha kubwa mchezaji huyo ambaye alicheza mechi yake ya kwanza kwa dakika 90 akiwa ndani ya jezi ya Liverpool.

 

Licha ya Kocha wa Liverpool, Jur­gen Klopp kufanya mabadiliko ya kikosi katika mchezo huo, bado lawama nyingi zinaonekana kumuan­gukia Chamberlain ambaye hajaonyesha makali tangu ameanza kupewa nafasi.

 

Katika mchezo huo Cham­berlain alipangwa kucheza nafasi ya kushambulia akitokea pembeni na siyo katikati kama ambavyo ame­kuwa akitaka, lakini kutokana na kiwan­go anachokionye­sha baadhi ya mashabiki wao w a m e a n z a kuhisi kuwa mchezaji huyo ana ‘gundu’ na kuanza kumlau­mu.

 

U p a n d e mwingine ni kuwa mashabiki wa Arse­nal nao wameanza kuwadhihaki wale wa Liverpool waki­waambia kuwa wamebeba mzigo ambao wao uli­washinda.

 

M c h e z o wake wa kwan­za akiwa Liv­erpool licha ya kuanzia b e n c h i , Chamber­lain al­ishuhu­dia timu yake ikipata kichapo cha mabao 5-0 kutoka kwa Manchester City, baadaye ikafuata sare ya mabao 2-2 dhidi ya Sevilla kati­ka Ligi ya Mabingwa Ulaya.

 

Baada ya hapo Liverpool ikapata sare ya bao 1-1 dhi­di ya Burnley katika Premier League.

Utani ambao umekuwa ukitawa­la kwenye mitandao ya jamii na mingine ya michezo ni juu ya kiwango cha Chamberlain ambapo thamani iliyotumika kumsajili na kile kina­choonekana uwanjani vinaoneka­na kuwa ni vitu viwili tofauti.

 

Kingine ni kuwa katika mchezo ujao wa wikiendi hii wa Liverpool ni kuwa wanatarajiwa kukutana na wapinzani wao haohao, Leices­ter City lakini safari hii ni katika Premier League, hivyo Liverpool italazimika kufanya kazi ya ziada kuwaamini­sha mashabiki wao k u w a tatizo siyo Cham­berlain.

 

Baadhi ya mashabiki wa Arsenal wamekuwa wakisema kuwa mchezaji huyo ana laana ya Wenger kwa kuwa ni kocha ambaye alichangia kumsimamia tangu alipomsajili akiwa chipukizi akitokea Southampton.

 

Wenger alimvumilia licha ya kuwa hakuwa katika ubora wa juu kama ilivyotegemewa lakini baada ya kuona mambo hayaendi vizuri na timu hiyo inapitisha mia­ka mingi bila kutwaa ubingwa wa Premier ameamua kuondoka

Mashabiki wengine wa Arse­nal wamesema kuwa mche­zaji huyo mwenye umri wa miaka 24 hana uw­ezo wa kutosha, hivyo kusajiliwa na Liver­pool ni sawa na ku­wapunguzia mzigo wao.

 

Shabiki mwingine akawazodoa kwa kusema kuwa Liverpool wa­likataa pauni milioni 100 za kumu­uza Coutinho kisha wakamsajili Chamberlain kwa pauni milioni 35 kitu ambacho ni kibaya kibiashara.

 

Hivyo, Liverpool inahitaji ush­indi katika wikiendi hii, kinyume na hapo presha itaendelea kuwa kubwa kwa Chamberlain ambaye pia ni mchezaji wa timu ya Taifa ya England.

Leave A Reply