TIMU ya masoko ya Kampuni ya Global Publishers, leo Jumamosi, Aprili, 24 2021, ilimwaga fedha kwa wasomaji wao waliokutwa wanasoma Gazeti la Championi ambalo huchapishwa na kampuni hiyo.
Wasomaji mbalimbali waliokuwa wakisoma gazeti hilo walirudishiwa fedha zao walizotumia kununua gazeti hilo. Promosheni hiyo ilifanyika maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Wasomaji walionekana kufurahia promosheni hiyo ambayo itakuwa endelevu kwa siku za Jumamosi. Wiki ijayo una nafasi ya wewe msomaji kurudishiwa fedha uliyotumia kununulia Gazeti la Championi linalouzwa Sh 800, kama utakutwa unasoma gazeti hilo.