Balaa la Twanga Pepeta Usiku wa Manane
BENDI ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ inayotamba na wimbo wake mpya wa Mapenzi Sigala Kali, usiku wa kuamkia jana (Jumamosi) ilipiga bonge la shoo ndani ya kiwanja cha Green Palm kilichopo Kunduchi Jijini Dar.
Shoo hiyo ilihudhuriwa na nyomi la mashabiki ambapo wapiga vyombo na wanenguaji walifanya makamuzi si ya kitoto.
Mnenguaji mwenye makeke mengi ambaye ni kiongozi wa wanenguaji wa bendi hiyo, Super Nyamwela na wanenguaji wake nao kama kawaida yao ilikuwa full kudatisha na mastaili yao mapya.
HABARI/PICHA:RICHARD BUKOS /GPL