Shoo ya Eid: Tazama Zuchu Alivyosepa na Kijiji Dar Live – Video
MWANADADA Zuchu anayetisha kunako gemu la Bongo Fleva kutoka lebo ya WCB usiku wa wa kuamkia leo alipiga bonge la shoo ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live.
Zuchu kabla hajapanda jukwaani kwenye ukumbi huo wa kisasa uliofurika nyomi kubwa la mashabiki alitanguliwa na wasanii kadhaa akiwemo mama yake mzazi Khadija Kopa na kundi lake la Ogopa Kopa.
Katika shoo mashabiki waliofurika ukumbini hapo walikuwa wakilipuka kwa mayowe ya kushangilia mwanzo mwisho.
HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS / GPL