Cheki Rose Manfere Alivyotwaa Taji la Miss Tanzania kwa Mbwembwe
Mrembo Rose Manfere usiku wa kuamkia leo ametwaa taji la Miss Tanzania kwa mbwembwe na mikogo akiwabwaga wenzake 19 katika shindano lililofanyika Ukumbi wa Mwalimu Nyerere uliopo Posta Jijini Dar.
Rose alianza kuonesha mikogo yake tangu walipoanza kupita jukwaani na kuonesha vipaji tofauti.
Katika mpambano huo mgeni rasmi alikuwa Naibu Spika wa Bunge, Akson Tulia ambapo akizungumza mbele ya wageni waalikwa alimuomba muandaaji wa mashindano hayo, Basila Mwanukuzi kuendeleza vipaji vya warembo wengine waliomfuatia Miss Tanzania huyo.
Mshindi huyo anayetarajiwa kuiwakilisha nchi kwenye mashindano ya dunia mwakani nchini Brazil, amezawadiwa gari aina ya Subaru.
Angalia picha