KLABU ya Inter Milan inatarajiwa kutuma ofa ya kumsajili kiungo Nemanja Matic wa Chelsea baada ya klabu hiyo kukataa kumuuza mchezaji huyo kwenda Manchester United.
Uhusiano wa United na Chelsea haupo sawa baada ya United kumsajili Romelu Lukaku wa Everton ambaye alikuwa akiwaniwa kwa ukaribu na Chelsea.
Taarifa kutoka Italia zinaeleza kuwa, Chelsea ipo tayari kumpeleka Matic Italia kuliko aende United hasa endapo itafanikiwa kumsajili Tiemoue Bakayoko wa Monaco ambaye anawaniwa na United