The House of Favourite Newspapers

CHRIS BROWN AGOMA KUKABIDHI SIMU YAKE KWA WAPELELEZI

Image result for chris brown

MWANAMUZIKI Chris Brown amekataa kukabidhi simu yake kwenye bodi ya upelelezi kwa ajili ya uchunguzi wa tuhuma za ubakaji dhidi ya mwanamke mmoja nchini Ufaransa.

 

Kwa maelezo ya nyaraka za mahakama imeeleza kuwa endapo Chris Brown atakabidhi simu yake kwa ajili ya upelelezi kuna uwezekano kutokua na usalama endapo mshtaki akifanya maamuzi ya kuchukua namba za simu ambazo ni za siri za watu wake wa muhimu.

 

Januari 22, 2019, Chris alishikiliwa na polisi kwa tuhuma za ubakaji nchini Ufaransa na kuwekwa rumande saa 24 na baadae aliachiwa huru na kurudi Marekani na pia aliwahi kukanusha taarifa hizo na kusema kuwa zilikua zikimchafua.

Comments are closed.