CHUO Kikuu Katoliki Ruaha (Ruaha Catholic University) kimetoa taarifa ya kufunga shughuli zake zote isipokuwa za dharura na kutoa likizo ya dharura kwa wafanyakazi wote kuanzia Mei Mosi, 2020. Aidha, wafanyakazi watalipwa nusu mshahara kwa mwezi Aprili, na chuo kitaziomba benki kusitisha makato ya mikopo.