MNADHIMU wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Ester Bulaya, ametangaza kuwa wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wamekubaliana kuanzia leo Mei 1, 2020, hawatoingia bungeni kuhudhuria vikao na watabaki nyumbani Dodoma kama tahadhari ya maambukizi dhidi ya ugonjwa wa COVID 19.