The House of Favourite Newspapers

D’banj afurahishwa na Kolabo ya Don Jazzy

0

Dbanji na Don jazMwimbaji maarufu wa Nigeria, D’banj (kulia) na prodyuza Don Jazzy

USEMI   kwamba ‘Sauti ya umma ni sauti ya Mungu’ umewaleta karibu mwimbaji maarufu wa Nigeria, D’banj na prodyuza Don Jazzy ili kukidhi hau ya mashabiki wao.

Hapa itakumbukwa kwamba mwimbaji maarufu wa Nigeria, 2Face Idibia aliwahi kushikamana na  mshikaji wake, Don Jazzy, na kuwapa mashabiki wao bonge la wimbo wa ‘Bangelee’.

Akielezea furaha yake katika matarajio ya  kolabo hiyo,  D’banj alisema, “Hivi sasa tumepanga bonge la ‘kitu’  ambacho nyie wapenzi wetu, mtakipenda, ni wimbo ambao mtausikia hivi karibuni.

“Ninaamini kwamba anayoyasema 2Face kwamba mambo yote ni sauti ya MUngu. Pia mfahamu kwamba tukio tulilopanga linaangukia katika kudhimisha mwaka wangu wa kumi katika tasnia hii, na ni mwaka wa kumi pia kwa Don Jazzy katika tasnia hii. Don Jazzy ni kaka yangu tumepanga kufanya vitu vikubwa zaidi,” alisema D’banj.

Leave A Reply