Denis Nkane Yamemkuta Yanga, Nje Mwezi
KIUNGO Mshambuliaji waYanga, Denis Nkane atakuwa nje ya uwanja kwa mwezi mmoja kutokana
na kusumbuliwa na Kinena.
Nkane alisajiliwa na Yanga kwenye dirisha dogo la usajili akitokea Biashara United, huku kwa sasa akiwa
amecheza mechi mbili za michuano ya Mapinduzi.
Kiungo huyo aliumia kwenye mchezo wa hatua ya makundi dhidi ya KMKM kwenye Kombe la Mapinduzi.
Akizungumza na Championi Jumatano, Daktari waYanga, Youssef Mohammed, alisema kuwa: “Kwa sasa kuna jumla ya wachezaji wanne ambao ni majeruhi kwenye kikosi.
“WapoYacouba Sogne, Kibwana Shomari,Abdallah Shaibu ‘Ninja’ ambao wanaenda Tunisia kwa ajili ya
kupatiwa matibabu na Denis Nkane.
“Denis alipata majeraha kwenye mchezo wa mwisho wa makundi ambapo kwa sasa anasumbuliwa na Kinena, tatizo ambalo litamuweka nje kwa muda wa mwezi mmoja.”
STORI NA LEEN ESSAU, Dar es Salaam