The House of Favourite Newspapers

Denti atoroshwa, awekwa kinyumba

0


Denti
Binti huyo anayedaiwa kuwekwa kinyumba.

Boniphace Ngumije
Dunia imekwisha! Binti mwenye umri wa miaka 14 (jina linahifadhiwa kimaadili), mkazi wa Majohe-Kwawarioba, Gongo la Mboto jijini Dar ambaye ni mwanafunzi (denti) wa kidato cha kwanza katika shule moja ya sekondari iliyopo maeneo hayo, anadaiwa kutoroshwa nyumbani kisha kuwekwa kinyumba.

Kwa mujibu wa mama mzazi wa denti huyo, Edna Zacharia, tukio hilo lilijiri hivi karibuni ambapo juhudi zote alizozifanya kumtafuta mwanaye huyo ziligonga mwamba huku tetesi za mhusika aliyetenda tukio hilo akiwa nazo.

Denti-3Mzazi huyo alisema kuwa binti yake huyo alianza kufanya jaribio la kutoroka siku moja kabla ya kutimiza azma yake ambapo tofauti na utaratibu wa kawaida, siku hiyo alirejea nyumbani kwa kujifichaficha.

Mama huyo aliendelea kueleza kwamba, baada ya kumhoji mwanaye, alimwambia alikuwa amepoteza shilingi 500 ya mama huyo, hivyo aliogopa kuonekana mbele yake akihofia kupewa adhabu.

Alisema alimsamehe mwanaye na akamwambia aende kulala na mdogo wake lakini kwa kuwa azma yake ilikuwa kutoroka, siku iliyofuata mama huyo aliporejea kutoka kwenye majukumu yake, hakumkuta na baadhi ya nguo zake hazikuonekana.

“Baada ya saa 24 niliripoti tukio hilo kwenye Kituo cha Polisi cha Majohe, nikaandikisha taarifa, tukaanza kumsaka usiku na mchana nikisaidiana na ndugu zangu, tulipata taarifa kuwa yupo kwa kijana muuza mkaa anayefahamika kwa jina la Issa anayeishi Mabibo-External (Dar), tukaenda polisi na kufunguliwa jalada namba STK/RB/1835/15 -KUTOROSHA BINTI CHINI YA HIMAYA YA WAZAZI),” alisema mama huyo.

Camillius-WamburaEdna alisema katika harakati za kumtafuta mwanaye huyo, aliwataarifu baadhi ya ndugu zake akiwemo kaka yake, Damian Ndelwa ambaye mkewe ndiye alikuwa anafahamu mahali alipoonekana binti huyo, ndipo wakakusanyana na baadhi ya watu wake wa karibu kisha kwenda kuvamia kwenye eneo la tukio.

Hata hivyo, mtuhumiwa na denti huyo walikimbia ndipo ndugu hao wakachukua uamuzi wa kwenda kituo cha polisi kilichopo karibu walikoambiwa waendelee kumtafuta kwa kuwa wana RB.

Kuhusu shuleni, Edna alisema mwalimu mkuu na walimu wengine walimshauri kwenda kutafuta msaada kwenye taasisi ya haki na sheria lakini alidai alipofika huko walimrudisha polisi wakimsisitiza kuendelea kumtafuta na kuripoti polisi ikiwa hatapatikana.

Mama huyo aliwaomba watu watakaomuona wawasiliane naye kupitia namba za simu zake za mkononi 0788 291 318, 0769 737 447 au 0672 506 746 au watoe taarifa kwenye kituo cha polisi kilichopo karibu,

Leave A Reply