The House of Favourite Newspapers

Diamond na Siri ya Kuvaa Msalaba

Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz

MWANAMUZIKI kiwango kwenye gemu la Muziki wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’, amefunguka kwamba watu wamekuwa wakimdis kutokana na kuvaa kwake cheni yenye msalaba bila kufahamu nini anamaanisha.

 

Akichonga na Mikito Nusu Nusu, Diamond alifunguka kwamba kwake huwa hachukulii cheni hiyo kama msalaba, bali ni alama ya jumlisha ambaye kwake inamaana kubwa ambayo ni siri yake.

 

“Cheni ninayovaa na watu kunidisi kwamba ni msalaba kiukweli huwa ninashangaa sana kwa maana watu huzungumza kile ambacho hawakifahamu. Kwangu huo si msalaba, bali ni alama ya jumlisha ambayo ninaona haina tatizo lolote, kwani alama hiyo inamaana kubwa kwangu ambayo itabaki kuwa siri yangu!” alisema Diamond.

STORI: BONIPHACE NGUMIJE

Comments are closed.