The House of Favourite Newspapers

Diva azidi kumuandama Mondi

0

 

 

MWANADADA aliyejizolea umaarufu kutokana na kazi ya utangazaji; Loveness Malinzi marufu kama Diva amezidi kumuandama Diamond ‘Mondi’ na sasa amemuita muongo mkubwa.

Hatua hiyo imekuja baada ya Diamond kunukuliwa na vyombo vya habari kuwa Diva anamchukia kwa sababu amekuwa akimsumbua kumuomba amuajiri katika kampuni yake ya habari ya Wasafi na kwamba amekuwa akimpotezea.

“Mimi siyo wa kuomba kazi Wasafi kwa Diamond, labda kama anataka umaarufu kupitia kwangu,” alisema Diva na kuendeleza marumbano na vijembe kati yake na Mondi ambavyo vimekuwa gumzo mitandaoni

Stori: Ammar Masimba, Uwazi

Leave A Reply