The House of Favourite Newspapers

DMX ASAINI MKATABA MPYA NA DEF JAM

 

KAMPUNI ya muziki ya Ruff Ryders imesaini mkataba mpya na Def Jam Records, kwa mujibu wa XXL. Mwaka 1998, mwanamuziki DMX  aliachia rekodi yake ya kwanza ya It’s Dark and Hell Is Hot katika lebohiyo na inashika namba katika mauzo miaka ya mwishoni ya 1990 na mwanzoni mwa 2000.

Katika kipindi hicho aliachia albam tano zikiwemo za  Flesh of My Flesh, Blood of My Blood  na mnamo 1999 aliachia And Then There Was X ambapo albam ya mwisho ilikuwa mwaka  2003’ ikiitwa  Grand Champ.

Swizz Beatz ilithibitisha utiaji saini huyo katika mahojiano na  “The Breakfast Club.

“Mambo yote yamesainiwa hivyo utakuwa mwaka wenye neema kwake, Mungu akipenda.  Atakwenda mahali ambapo amekuwa anataka kwenda,” alisema ofisa mmoja wa lebo hiyo.

 

 

Comments are closed.