The House of Favourite Newspapers

DPP Afafanua Alivyomtoa Gerezani Kada CHADEMA

0

MKURUGENZI wa mashtaka nchini Tanzania (DPP), Biswalo Mganga, leo Jumatano Desemba 2, 2020, ameeleza kuhusu uamuzi wake wa kumfutia mashtaka kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Nusrat Hanje,  ambaye Novemba 27, 2020 alivuliwa uanachama wa chama hicho pamoja na wenzake 18.

 

Akizungumza na wanahabari katika Gereza Kuu la Karanga mjini Moshi, Mganga amesema alimwachia kada huyo kwa mamlaka aliyonayo chini ya kifungu cha 91 cha Kanuni za Makosa ya Jinai cha mwaka 2002.

 

 

Ametoa kauli hiyo wakati akitoa taarifa ya kuwafutia mashtaka watuhumiwa 72 ambao walikidhi sifa za kufutiwa mashtaka kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo za kubambikiwa makosa.

Leave A Reply