DRC: Upinzani Waitisha Maandamano Nchi Nzima Siku Ya Kuapishwa Rais Tshisekedi
Viongozi Watatu wa Upinzani wameitisha maandamano ya Nchi nzima kuanzia Januari 20, 2024, siku ambayo Félix Tshisekedi anatarajiwa kuapishwa na kuendelea na Urais kwa Awamu ya Pili
Wito huo umetolewa na mmoja wa waliokuwa wagombea, Moise Katumbi ambaye kwa mujibu wa matokeo ya Tume ya Uchaguzi ya DR Congo (CENI) alipata 18% akiwa pamoja na wenzake Martin Fayulu (5%) na Anzuluni Bembe (1%) wakidai kulikuwa na udanganyifu na wizi wa kura katika uchaguzi wa Desemba 2023
Aidha, Tshisekedi ameshinda uchaguzi kwa 73% ya kura kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi lakini matokeo hayo yamekuwa yakipingwa na upande wa Upinzani unaotaka Uchaguzi urudiwe