ESMA: NITACHANGUA MWANAUME KAMA KARANGA
BAADA ya kuachana na mumewe, dada wa mwanamuziki maarufu wa Afro-Pop, Nasibu Abdul ‘Diamond Platinumuz’, Esma Khan amefunguka kuwa amejifunza pindi atakapoamua kuingia tena kwenye uhusiano ni lazima atakuwa akichagua mwanaume kama karanga ili angalau ampate mwenye uaminifu.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Esma alisema amekuwa akiumia na kuvumilia muda mrefu kwenye ndoa yake hiyo ya yeye na mumewe, Hemed Manungi ‘Petit Man’ kabla ya wawili hao kutengana.
“Unapoumwa na nyoka lazima ukiona hata jani unashtuka sana na ndiyo yamenikuta. Sasa hivi mwanaume lazima nimkague sana hata mwaka mmoja ndiyo niweze sasa kuolewa naye au hata kuwa wapenzi vinginevyo hapana, siwezi,” alisema Esma
STORI: IMELDA MTEMA, DAR
Comments are closed.