Awali ilionekana, huenda Baraka angechukua nafasi hiyo na kuwa katibu kamili wa Yanga, hata hivyo ikaonekana hakuwa amefanya utendaji katika kiwango kilicho sahihi kama ambavyo uongozi wa Yanga ulitarajia.
DAR ES SALAAM: ALIYEKUWA Kocha Mkuu wa Timu ta Taifa Tanzania ‘Taifa Stars’ Charles Boniface Mkwasa ameteuliwa na kutangazwa kuwe Katibu Mkuu mpya wa Klabu ya Yanga kuchukua nafasi ya Baraka Deusdedit ambaye anashushwa na kuwa mhasibu wa klabu hiyo.
Mkwasa ambage aliwahi kuwa kocha msaidizi wa Yanga na baadaye Kocha Mkuu wa Taifa Stars, huenda ametangazwa rasmi leo Januari 31 kuchukua nafasi hiyo.
Aidjha imeelezwa kuwa, Charles Boniface Mkwasa rasmi ataanza kazi rasmi kesho katika nafasi yake ya Katibu Mkuu mpya Yanga.
Mkwasa anakuwa mchezaji mwingine wa Yanga baada ya Lawrance Mwalusako kushika wadhifa huo wa utendaji.
Wakati akiwa mchezaji, alikuwa kiungo nyota wa Yanga na Timu ya Taifa Stars.
Yanga inatarajia kumtangaza leo na Mkwasa atachukua nafasi ya Baraka Deusdedit aliyekuwa akikaimu nafasi hiyo ambaye imeelezwa anashushwa na kuwa bwana fedha.
Global Publishers and General Enterprises Limited is a registered private company dealing in publishing of weekly Swahili newspapers in Tanzania, namely; Uwazi, Ijumaa, Championi, Amani, Risasi & Ijumaa Wikienda.
Comments are closed.