The House of Favourite Newspapers

Familia ya Ronaldo Yashutumu Madai ya Ubakaji Dhidi Yake

Related image

FAMILIA ya mwanasoka raia wa Ureno na klabu ya Juventus ya Italia, Cristiano Ronaldo,   imeshutumu  vikali madai dhidi yake, ambapo dada yake, Katia Aveiro,  na mama yake, Dolores Aveiro,  wame-post picha yake na ujumbe mbalimbali kuhusu suala hilo kwenye mitandao ya Facebook na Instagram.

“Ninataka kumwona mtu aliye na ujasiri wa kuiweka picha hii katika mitandao na kumvunjia heshima… kuivunjia heshima Ureno na umoja wa watu wetu wa kupigania haki,” yalisema maelezo kwenye picha hiyo.

Picha hiyo ina maelezo mengine mawili kwa Kireno, moja ikisema “#Ronaldo, tuko na wewe hadi mwisho” nyingine  “Haki itendeke kwa CR7”.

Ronaldo amefunguliwa mashitaka ya ubakaji na Kathryn Mayorga anayedai alimshambulia katika hoteli moja huko Las Vegas, Marekani,  mwaka 2009. Mayorga aliongeza kwamba Ronaldo alimlipa Dola 375,000 kumtaka asilitangaze jambo hilo.

Nyota huyo wa soka amesema madai hayo ni ya uwongo.

Credit: Bella Naija

Comments are closed.