Matokeo ya kidato cha sita kwa mwaka 2017 yametoka leo Jumamosi, Julai 15 huku shule ya Wasichana ya Feza Girls ikiibuka kinara kwa watahiniwa wake 67 kufaulu kwa kupata daraja la kwanza na la pili.
Shule nyingine ni Marian Girls (Pwani) iliyoshika nafasi ya tano, Mzumbe (Morogoro) nafasi ya sita, St Marry Mazinde Juu (Tanga) nafasi ya saba, Tabora Boys (Tabora) nafasi ya nane, Feza BOYS (Dar es Salaam) nafasi ya tisa na Kibaha ya Pwani iliyoshika namba kumi.
Tazama Orodha ya Shule 10 Bora
- Feza Girls
- Marian Boys
- Kisimiri
- Ahmes
- Marian Girls
- Mzumbe
- St Marry Mazinde Juu
- Tabora Boys
- Feza Boys
- Kibaha
Shule nyingine zilizoibuka kidedea katika matokeo hayo ni Marian Boys, iliyoshika nafasi ya pili, Kisimiri (Arusha) imeshika nafasi ya tatu na Ahmes (Pwani) imeshika nafasi ya nne.
NECTA Yawafutia Matokeo Wanafunzi 10 wa Kidato cha Sita
Vinara wa Matokeo Kidato cha Sita Hawa Hapa