The House of Favourite Newspapers

Fiston Awapoteza Chama, Luis Bongo

0

LICHA ya kwamba mtambo mpya wa mabao wa Yanga, Fiston Abdoul Razak bado haujaja Bongo kwa ajili ya kuanza majukumu yake, lakini tayari amewagaragaza vibaya mastaa wanne wa timu ya Simba.

 

Nyota huyo raia wa Burundi, amewaacha mbali nyota hao wa Simba ambao ni Meddie Kagere, Bernard Morrison, Luis Miquissone, John Bocco na Clatous Chama.Fiston amewakalisha nyota hao kwenye suala la thamani ambapo kwa mujibu wa Mtandao wa Transfermarkt, ambao unajihusisha na data mbalimbali za wachezaji ulimwenguni, Mrundi huyo sokoni ana thamani ya Euro 270,000 (sawa na Sh 752,663,000).

 

Mrundi huyo ambaye amesajiliwa kwa mkataba wa miezi sita ndani ya Yanga, thamani yake hiyo inaonesha ilifanyiwa maboresho Novemba 12, 2020 ambapo alikuwa akikipiga ENPPI ya Misri.Thamani hiyo inamfanya Fiston kuwaacha Luis mwenye thamani ya euro 135000 (Sh 376,331,000) ikiwa mara ya mwisho rekodi zake kuboreshwa ni Juni 2, 2018.

 

Pia amemuacha Chama ambaye thamani yake ni Euro 90000 (Sh 250,888,000) ikiwa mara ya mwisho rekodi zake kuboreshwa ni Januari 11, 2017.Kagere thamani yake ni Euro 90,000 (Sh 250,888,000), John Bocco Euro 135000 (Sh 376,331,000) na Bernard Morrison Euro 175000 (Sh 487,837,000).

 

Kinara ambaye anaongoza kwa kuwa na thamani ya juu katika Ligi Kuu Bara ni Saidi Ntibazonkiza ‘Saido’ wa Yanga mwenye Euro 49,5000 (Sh 1,379,880,000)

Leave A Reply