KITUNZA data aina ya (Flash Disk) chenye orodha ya majina ya wafanyabiashara wakwepao kodi imeibua gumzo Ikulu baada ya Rais John Magufuli kujikagua kila kona ya mifuko ya nguo aliyoivaa bila kuiona.
Magufuli leo Juni 7, amekutana na kufanya mazungumzo na wafanyabiashara wakubwa 1,000 kutoka wilaya zote 139 nchi nzima, Ikulu jijini Dar es Salaam na kusema kuwa changamoto za ukwamishaji wa biashara kwa upande wa serikali ni kutokana na utitiri wa taasisi za udhibiti.
Aidha, ameongeza kuwa zipo taasisi nyingi za udhibiti ambazo zinaingiliana kimajukumu, kwa mfano TBS, NEMC, WAKALA WA VIPIMO, TUME YA USHINDANI, EWURA, SUMATRA, TFDA, OSHA, OFISI YA MKEMIA MKUU, Na kadhalika.
Comments are closed.