The House of Favourite Newspapers

YANAYOJIRI GYMKHANA BUKOBA KWENYE MAZISHI YA RUGE – PICHAZ

Licha ya huzuni kuwatawala lakini walihakikisha wanafanya kile ambacho Baba yao anakipenda kuwaona wanafanya kwa wakati wote. Watoto wa Ruge Mutahaba (Wasanii wa THT) Wakimuimbia Baba yao ambaye amelala usingizi mzito mbele yao.

MWILI wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media, marehemu Ruge Mutahaba umeagwa katika ibada maalum iliyofanyika kwenye viwanja vya Gymkhana Bukoba mkoani Kagera.

Viongozi mbalimbali wamejitokeza kuaga mwili wa Ruge wakiwemo Mawaziri, wabunge, viongozi wa vyama, dini, wasanii, ambao kwa pamoja wameungana na ndugu, jamaa, marafiki na wakazi wa Bukoba kuusindikiza mwili wa Ruge katika nyumba yake ya milele.

Baada ya shughuli za kuaga mwili wa marehemu Ruge Mutahaba kumalizika katika viwanja vya Gymkhana, tayari safari ya kuelekea Kijijini kwao Kiziru-Kabale kwaajili ya maziko imeanza.

 

“Kama kila mmoja aliyeguswa hapa ataamua kusaidia angalau Watanzania wawili/watatu pengo lake linaweza kuzibwa” – Mwachi Mutahaba.

 

“Upendo, uthubutu na kujiamini zilikuwa ni tunu zilizomsaidia kufanya aliyofanya… amefanya mengi na kugusa mengi.” – Waziri Kairuki. Waziri Kairuki amesema Serikali inasikitika kwamba kifo cha Ruge Mutahaba kimetokea katika wakati ambapo moto wa uchumi wa viwanda na fursa za kibiashara umekolea katika nchi yetu wakati yeye alikuwa mwanga na dira ya wengi katika kuziendea Fursa.

 

Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete akisalimiania na Nape Nnauye katika ibada ya kuaga mwili wa Marehemu Ruge Mutahaba kwenye vinja vya Gymkhana Bukoba….

 

Mrisho Mpoto akiimwita Ruge Mutahaba kwa sauti ya juu zaidi ya mara nne akitegemea atainuka lakini aikuwa hivyo ameimba kwa machungu sana.

 

 

Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe akitoa salam za pole kwa ndugu na familia ya Ruge.

 

Harmonize msibani kwa Ruge.
Alikiba na meneja wake, Seven Mosha.

 

Wasanii mbalimbali waliosafiri kutoka DSM na maeneo mengine kuja Bukoba kumsindikiza Ruge Mutahaba katika safari yake ya mwisho. .

 

 

 

“Kama watoto wamsubiriavyo Baba nyumbani, ndivyo tulivyokuwa tukimsubiri Ruge kila jioni pale THT. Kwa miaka 15, hajawahi kuacha kuja” – Lameck Ditto

 

“Ruge hakuwa kwenye sehemu moja tu ya sanaa (aliwagusa Bongo Movie kwa kiasi kikubwa) Tutachukua mazuri yote ya Ruge tutakwenda nayo, asante Ruge” – Steven Nyerere.

 

Nguvu za kusimama hana, bado anatafariki mshumaa kuzimika mapema, Taifa linasononeka.

 

iongozi mbalimbali wa serikali wakiwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa CMG, Joseph Kusaga wakiwa hapa viwanja vya #Gymkhana katika ibada ya mwisho ya mpendwa wetu Ruge Mutahaba.

 

Rita Paulsen, Mmiriam Odemba futeni machozi, msilie kwani yeye kasema akitangulia tusilie bali tusherehekee japo ni ngumu kufurahi wakati mioyo yetu inavuja jasho la huzuni.

 

Comments are closed.