Toyota Spacio Yapata Ajali Sinza, Dar
GARI dogo aina ya Toyota Spacio leo jioni limepata ajali baada ya kuacha barabara na kuingia mtaroni eneo la Sinza-Mori jijini Dar es Salaam na kuharibika kwa kiasi kikubwa. Hata hivyo, hakuna mtu aliyeumia licha ya uharibifu wa gari hilo na kibanda cha biashara kilichokumbwa na gari hilo.
Mashuhuda wa ajali hiyo walisema chanzo cha ajali ni mwendo kasi wa dereva wa gari hilo ambapo ghafla alikutana na mwendesha bodaboda na wanafunzi watatu mbele yake, hivyo katika kuwakwepa alijikuta gari likimshinda na kupoteza mwelekeo kisha kuingia mtaroni na kugeukia lilikokuwa likitoka.
Comments are closed.