KAMA kawaida, leo tena timu ya wafanyakazi wa Global Publishers, wakiwemo wahariri wa magazeti ya kampuni hiyo, wameingia mitaani kuendelea kulinadi gazeti la michezo la Spoti Xtra ambalo ni jipya lililoingia mitaani Alhamisi ya wiki iliyopita kwa bei ileile ya shilingi 500.
Akizungumzia ujio huo wa gazeti la Spoti Xtra kila Alhamisi, Mhariri wa Gazeti la Ijumaa Wikienda, Sifael Pau, amesema kwa wapenzi wa habari za michezo gazeti hilo ndiyo sehemu sahihi ya kumaliza kiu yao ya habari za michezo, hivyo walinunue gazeti tena kwa bei ileile ya sh. 500 tu.
Nao baadhi ya wasomaji wa gazeti la Spoti Xtra ambao walichangamkia kulinunua maeneo ya stendi ya mabasi yaendayo mikoani Ubungo, wamelipongeza kwa mwonekano mzuri na kwa namna ambavyo limesheheni habari za michezo na hivyo wakasisitiza juu ya kulinadi kwa wingi mtaani ili kila mpenda soka kuweza kuliata.
“Global mmetusaidia kuliingiza gazeti hilo siku ya Alhamisi kwani tumekuwa tukikosa habari za michezo kwa siku hiyo, hivyo endeleeni kulisambaza kila kono ya nchi ili wadau wapate habari za michezo,” alisema mmoja wa madereva wa stendi hiyo aliyejitambulisha kwa jina la Abubakar Juma.
Matukio katika Picha:
Comments are closed.