The House of Favourite Newspapers

Mbunge Awapa Yanga Ushindi

Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete.

MWANACHAMA na mpenzi wa klabu ya Yanga ambaye pia ni Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete, amesema kuwa haoni sababu zozote zitakazowazuia Yanga kukosa ushindi kwenye mechi dhidi ya Simba.

 

Yanga na Simba zinavaana Jumpili hii kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara, mchezo ambao unasubiriwa kwa hamu kubwa sana.

Ridhiwani ambaye ni mwanachama na mpenzi mkubwa wa klabu ya Yanga amesema timu yake ina uwezo mkubwa wa kupata ushindi kwenye mchezo huu.

 

Akizungumza na Spoti Xtra, Ridhiwani amesema Yanga imeimarika kwa sasa baada ya kushindwa kuanza vizuri na anaamini kuwa inaweza kupata ushindi mnono Jumapili.

 

“Kwa sasa Yanga ipo vizuri sana kama unavyoona kila nafasi ina mtu zaidi ya mmoja, imekuwa na kikosi kipana tofauti na msimu uliopita, naamini kuwa hii ni timu bora na itaibuka na ushindi kwenye mchezo ujao,” alisema Ridhiwani mtoto wa rais wa awamu ya nne, Jakaya Kikwete.

STORI NA ISSA LIPONDA | SPOTI XTRA

Comments are closed.